MAELEZO PODCASTS
Sikiliza MAELEZO PODCASTS (Podcasts za Kiswahili kutoka Idara ya Habari MAELEZO, Tanzania) kupata taarifa na matukio mbalimbali nchini Tanzania. Idara ya Habari (MAELEZO) ipo chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ikiwa na jukumu la kutoa taarifa kuhusu utekelezaji wa Sera, mipango na miradi ya maendeleo vinavyotekelezwa na Serikali kwa wananchi, kusimamia vyombo vya habari hasa magazeti na machapisho na kuishauri Serikali juu ya Sera na Sheria za habari.
Episodes
21 episodes
Tahadhari ya Mvua za El Niño Kuanzia Oktoba, 2026
Kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) juu ya uwepo wa mvua kubwa za El Nino, kupitia Maelezo Podcast ili kupata ufafanuzi tumezungumza na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang'a ambaye anaeleza k...
Aina Tatu za Saratani Zinazoathiri Maisha ya Wengi Nchini.
Katika kujenga uelewa kuhusu ugonjwa wa saratani, kupitia Maelezo Podcast tumemualika Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI), Dkt. Chrispin Kahesa, tumezungumza kuhusu saratani na namna inavyoathi...
Changamoto ya Afya ya Akili, ni Akina Nani Waathirika Zaidi?
Kupitia Maelezo Podcast tunajadili kuhusu afya ya akili kwa kumualika Daktari Veronica Lyimo, Bingwa wa Afya na Magonjwa ya Akili kutoka Taasisi ya Afya ya Akili Tanzania, ambaye anatupitisha kwenye visababishi vya changamoto ya afya ya akili, ...
Kwanini ni marufuku kutunza kwa kutupa fedha chini?
Mazungumzo na Bw. Atufigwege Mwakabalile, Afisa Mwandamizi wa Benki kutoka Benki Kuu Tanzania (BOT) kuhusu sheria ya fedha nchini na marufuku iliyotilewa ya kutotunza fedha kwa kutupa chini.
Sheria ya Kuasili Mtoto (Child Adoption) Tanzania
Kupitia MAELEZO PODCASTS leo tunazungumza na Bi. Ludovicka Samare, Afisa Ustawi Mwandamizi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, anatupitisha kwenye utaratibu na Sheria ya kuasili mtoto (Child Adoption), nchini Tanzania
Elimu ya Hisa, Hati Fungani, Uwekezaji
Mazungumzo na Imani Mhingo, Mtaalamu wa Elimu ya Fedha na Mitaji ya dhamana kutoka Benki ya CRDB kuhusu elimu ya hisa; nani anatakiwa kuwa na hisa? uvumi upi usio wa kweli kuhusu hisa? Angalizo na namna ya kutengeneza faida kwa njia ya umiliki ...
Tiba ya Upandikizaji wa Uume kwa Wanaume
Dkt. Rugakingira kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma anatupitisha kwenye huduma hii iliyojizolea umaarufu ya upandikizaji wa uume kwa wanaume wenye changamoto za uzazi. Amejibu kuhusu nani anaweza kupandikiziwa uume, gharama na matarajio...
Ukweli Kuhusu Faida za Vyama vya Ushirika
Mazungumzo na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika kutoka Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania, Bw. Florian Haule kuhusu ushirika na ukweli wake vile umesaidia kuinua uchumi wa Watanzania tangu zamani hadi sasa.
Fursa kwa Watanzania Kuelekea AFCON 2027
Kuelekea Michuano ya AFCON 2027 ambayo Tanzania anatarajiwa kuwa mwenyeji wa michuano hii mikubwa Barani Afrika, tumemualika Bw. Allan Allex, Afisa Michezo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Michezo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, am...
Siri ya Tarehe 7 Julai na Historia ya Tanzania Iliyowafanya UNESCO kuichagua kuwa Siku ya Kiswahili Duniani
Mazungumzo na Profesa Rehema Erasto., Mhadhiri wa Kiswahili kutoka Idara ya Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma kuhusu historia ya siku ya Kiswahili Duniani, nafasi ya lugha za kijamii (makabila), makosa kwenye lugha ya kiswahili na namna ya kusah...
Kwanini Kongamano la Kiswahili Ufaransa na si kwingine? Majibu ya Msemaji Mkuu wa Serikali
Gerson Msigwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo; na Msemaji Mkuu wa Serikali akitoa majibu ya ni kwanini Kongamano la Kiswahili la Pili la Kimataifa limefanyika nchini Ufaransa na si kwingineko.Pia tumezungumz...
Kuelekea Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa, Paris - Ufaransa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inatarajia kufanya Kongamano la pili la kimataifa la Kiswahili kati ya Julai 4 - 7, 2026, jijini Paris, Ufaransa...
Fursa, Ushirikiano kati ya Algeria na Tanzania: Balozi Matinyi
Mheshimiwa Balozi Mobhare Matinyi akizungumza mara baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho wa kibalozi kwa Mheshimiwa Abdelmadjid Tebboune, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, katika hafla iliyofanyika kwenye Ikulu ya Algier...
Balozi Kombo Aeleza Umuhimu wa Ziara ya Rais Samia katika Kuimarisha Mahusiano ya Tanzania na Urusi
Mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 7 Juni, 2026.
Miaka 10 ya BMH: Jinsi Hospitali ya Benjamin Mkapa Ilivyobadilisha Huduma za Kibingwa Tanzania
Hospitali ya Benjamin Mkapa ni hospitali ya rufaa ya kanda iliyopo jijini Dodoma, iliyoanzishwa kwa lengo la kutoa huduma za kibingwa ambazo kwa sasa zipo 20 na ubingwa bobezi zipo 17 kwa wananchi wa Tanzania na nchi jirani.
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 (Mei 4, 2026)
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, akiwasilisha makadirio ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Mei 4, 2026, bungeni, jijini Dodoma.
Hotuba ya Mhe. Rais Samia na Mhe. Rais, Paul Kagame, Mei 03, 2026
Rais wa Rwanda, Mhe. Paul Kagame, amefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania, akizungumza na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa...
Hotuba ya Rais, Dkt. Samia Kwenye Kongamano la Biashara Baina ya Tanzania na Kenya, Mei 4, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Kongamano la Biashara baina ya Tanzania na Kenya (Tanzania & Kenya Business Forum 2026), tarehe 04 Mei, 2026, JNICC, jijini Dar es Salaam ambapo kongamano hi...
Elimu kuhusu ugonjwa wa Seli Mundu na Dkt. Catherine Mhando
Pata ufahamu sahihi kuhusu chanzo, dalili, matibabu pamoja na kinga ya ugonjwa wa Seli Mundu (Sickle Cell) na Dkt. Catherine Mhando wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma.
Elimu kwa umma kuhusu zoezi la SENSA YA WATU NA MAKAZI (2022)
Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 ni kwa ajili ya mipango jumuishi na maendeleo endelevu ya nchi na yataongeza uwazi katika kugawa rasilimali zilizopo kuendana na uwiano wa idadi ya watu katika ngazi zote za utawala. Halikadhalik...